Sunday, December 7, 2014

FARAJI KONDO.

Kaka mkubwa mwenyewe. Hakuna wa kubisha kuwa Mazengo tunawakilisha na tunatisha. Popote utakapoenda uliza kuhusu Mazengo, utapelekwa hadi kwa Waziri. Unashangaa nini? Mazengo tumetoa Mawaziri.
Huyu ni mtarajiwa.

NI FURAHA TU!

Tunune kwa sababu gani sasa? Tumefundishwa maadili mema, hatuibi cha mtu, hatukabi, hatudanganyi ili tupate cha juu, hatuna mapozi, tunasaidiana. Kwa nini tusiwe na furaha?
Tacheni Wanamazengo tujiachie kwa matabasamu mwananaaaaaa.

ROMANA & RAWLING.

NI RAHA ILIYOJE?

Hakuna kama Mazengo aiseee. Wanafunzi tusio na papara ya maisha, ni furaha tele ndiyo iliyotawala katika maisha yetu.
Pongezi zije kwako dada yetu mpendwa.

ERIC MTUI

Moja ya wanafunzi mahiri kupata kutokea katika shule msingi Mazengo.
Mungu akuzidishie kila pumzi ambayo ambayo unaiomba kwake.

EDWIN JAMES & DIANA MINJA

Jimwayeni mwayeni bwana. Hakuna anayewabugudhi, sisi ni wamoja na tutaendelea kuwa pamoja daima. Wala hatuna papara.

Mazengo Oyeeeee.

ALLY YASIN

Kijana mtanashati kutoka Mazengo Shule ya Msingi. Maisha ni kama raha sana kama ulipita Mazengo Shule Ya Msingi.

Shukrani ziende kwa Waalimu wote waliomfikisha kijana huyu hapa. Bila nyie asingeweza kuandika Mama wala Baba.
Heshima na Nidhamu, ninyi ndio wa kupewa pongezi.
Asanteni Walimu wote wa Mazengo.

KIKAO CHA DODOMA, 2014

Wakati Dar es Salaam wanakutana, pia Mjini Dodoma baadhi ya wanafunzi wa Mazengo walikutana kwa pamoja na kujadili mambo kadha wa kadha katika kusukuma gurudumu la Muungano wa wanafamilia hii kubwa.
Hakuna Kama Mazengo Shule Ya Msingi bwanaaaaa.

Kama unabisha, hatubishani, leta hoja mezani tujadiliane kwa mifano hai. Mfano wetu huu hapa unaouona.

UKUMBUSHO.

LILIAN MSELE.
Katika ukumbusho huu wa kipekee, mwanadada huyu kaweza kuifanya Mazengo leo hii inaonekana mbele yenu.
Heshima nyingi zije kwako dada yetu.

KIKAO CHA KWANZA CHA WANAMAZENGO DAR ES SALAAM

Ilikuwa ni furaha sana kwa nyuso hizi kukutana na kutulia kwa pamoja tena mwaka 2014 baada ya kupoteana kwa muongo mmoja.

Shukrani za dhati zimuendee MUNGU baba mwenyezi kwani katika yeye hakuna kitakachoshindikana.
MAZENGO DAIMA.
KIONGOZI wetu, Dada yetu. Witness Peter.
Huyu ndiye aliyewaunga wanamazengo 2003 na kuwaweka pamoja hadi wanafikia hapa leo.

Hongera Dada.
Mwanamazengo 2003. LUCY.
Hongera Dada yetu